Saturday, August 25, 2012

Virunga at Afrikafest in July 2012

Lovely video clips of Virunga's performance at Afrikafest in Hertme, Netherlands in July have just been made available courtesy of Ton Kraayenvanger. Here is the sebene from "Malako" to start things off: special thanks to Peter Toll! Bandmembers were Syran Mbenza & Bopol Mansiamina on guitars, Amed Barry, bass, Komba Bellow Mafwala, drums, Roger Kom, sax, Ballou Kanta, harmony vocals & animation; Samba Mapangala, lead vocal/bandleader. Enthusiastic audience participation and ambiance from Kenyan community in Holland. Enjoy!

http://youtu.be/itno6a4oBGE

Saturday, May 19, 2012

Life Is Sweet - Summer Tour 2012

Gearing up now for performances in England, Netherlands and Los Angeles, CA, in June-July! Samba has not appeared in UK since 2007 at WOMAD, and a short tour of England in 2006 promoting the Song & Dance album, so we are looking forward to meeting and greeting his many many fans at events including Africa Oye in Liverpool (2 days, performing June 23 and June 24--free admission), and AfrikaFestival in Hertme, Netherlands July 8, as well as other gigs in and around London. And hang tight, Los Angeles: Virunga kicks off the Skirball Cultural Center's summer Sunset Concerts series on Thurs. July 26! Full details at our Facebook fan page and ReverbNation .

Tuesday, January 24, 2012

Dunia Tuna Pita Live on stage at Sauti za Busara 2009




Lighting up the stage in front of a Zanzibari crowd who seemed able to sing along to every song, this is Samba Mapangala peforming 'Dunia Tuna Pita' which translates as 'We are just passing through this world'. Recorded at Sauti za Busara 2009. Featured instrumentalists Syran Mbenza, lead guitar, Komba Bellow, drums. Produced by Andy Jones, Screenstation, for Busara Promotions.

Saturday, January 21, 2012

Malako on soundtrack for award-winning documentary "The People The Rain Forgot"



Director Sophia Tewa's film was awarded Best Documentary Feature at the 2012 Los Angeles Cinema Festival of Hollywood. The People The Rain Forgot tells the story of the most vulnerable victims of climate change in Africa. Drought haunts Kenya, ruining the livelihoods of millions. Whether it is man-made or the punishment of God, Kenyans don't agree. But the cause is widely known: the earth's climate is changing, fast. Pastoralists and farmers have to find new ways to survive as once-fertile lands are slowly turning into deserts. 2011.


Sophia Tewa is a New York-based journalist. She has worked with CNN and CBS. She teaches multimedia production at The Meridian, Lehman College. The People The Rain Forgot is her first documentary as a director and producer.

Monday, December 12, 2011

The many faces of "Vunja Mifupa"

It seems Samba's "Vunja Mifupa" will live forever. Here it is on an "American Idol"-type talent show in Nairobi performed by one Nga'nga'lito in 2009: http://youtu.be/465erYIKJj0
 
 

Friday, December 9, 2011

Vunja Manyumba

You will NOT believe this! Nairobi's political satire TV program XYZ Show has used "Vunja Mifupa" as the basis for this week's episode, to hilarious results! http://youtu.be/TbWXq8Miiz0
 
 

Thursday, December 8, 2011

Samba's BIG news in Tanzania!

http://www.mwanaspoti.co.tz/wcreadnews.php?id=9451

Mapangala bado ajivunia A/Mashariki

Samba Omar Mapangala
ANTHONY NYONGESA
LICHA ya kupiga hatua kubwa barani Ulaya anakoishi, mwimbaji, Samba Omar Mapangala, bado anayo mapenzi makubwa kwa Afrika Mashariki.

Hii ndiyo sababu ya yeye kurudi kurekodi nyimbo zake au kutunga vibao kusifia mandhari ya eneo hilo.
Kibao chake cha juzi cha �Zanzibar�, ni uthibitisho tosha kwamba Mapangala hayupo tayari kuisahau kanda hiyo kwa vyovyote.

Wimbo huo ulipigwa picha katika kisiwa cha Zanzibar akimshirikisha mwimbaji mkongwe, Bi. Kidude na msanii wa Kenya, Mike Awilo, wa kikundi cha Jamnazi Afrika.

Zanzibar, Tanzania na Kenya ni sehemu ambazo nimekulia, hivyo basi ni vigumu kwangu kuzisahau kwa urahisi,� anasema mwimbaji huyo.

Wimbo huo wa Zanzibar aliurekodi mwezi Septemba katika mataifa tofauti ya Afrika Mashariki. Tayari kibao hicho kimeanza kutamba.

Wimbo huo utaorodheshwa kwenye albamu ya Maisha Matamu anayotazamia kuizindua mapema mwakani atapofika jijini Nairobi kwa shughuli hiyo.

Kwenye wimbo Zanzibar, ninasimulia uzuri wa watu wa eneo hilo ambao ni wakarimu mno. Nilionyeshwa ukarimu wao mara ya mwisho nilipoenda huko kufanya shoo ya mwisho katika tamasha la Sauti za Busara mnamo 2009, alisema Mapangala alipohojiwa na Mwanaspoti jijini Nairobi hivi karibuni.

Mapangala ndiye aliyetunga vibao maarufu vya zamani kama vile �Vunja Mifupa�, �Karibu Kenya�, �Ujumbe� na �Nyama Choma�.

Kwa muda wa miaka 13, msanii huyu amekuwa akiishi Marekani anakoandaa shoo zake katika majimbo mbalimbali.
Kwenye wimbo Maisha Matamu ambao pia utabeba jina la albamu mpya, msanii huyo anaangazia kuhusu namna maisha yalivyo mafupi japo kuna mambo mengi mazuri.

Akizungumzia bendi yake ya zamani ya Orchestra Virunga ambayo ilivunjika mwaka 1993, Mapangala anasema ataifufua hivi karibuni.

Tangu kuvunjwa bendi hiyo, amekuwa akiwategemea wasanii wa kukodi, jambo analosema sasa linakaribia kufika ukingoni.

Kenya kuna wasanii mahiri mno, hivyo nikiwa Nairobi nitaandaa mipango kuhusu namna nitakavyoweza kuifufua bendi,alisema akizungumzia Virunga iliyotamba miaka ya 1980 na 1990.

Miaka miwili iliyopita, Mapangala, alinukuliwa kwenye vyombo vya habari akisema anatarajia kurudi Kenya kuendeleza maisha yake, anasemaje kuhusu hilo

Ni kweli, ninajiandaa kurejea nchini kikamilifu. Hata hivyo, sijaamua ni lini iwe hivyo. Kwa sasa ni kwamba niko mguu mmoja Nairobi, mwingine Marekani, kuna mambo kadhaa ninayolenga kutimiza kule pia,� alisema Mapangala.

Miongoni mwa hayo ni mipango yake ya kuuvumisha mtindo wa rhumba katika mataifa ya Magharibi, ili uwe maarufu kama ilivyokuwa Afrika Mashariki miaka 1980.

Mapangala mwenye umri wa miaka 55, anasema awali mtindo huo ulivumishwa Ulaya na mapromota kadhaa akiwamo Oluoch Kanindo aliyevisaidia vikundi kama vile Shirati Jazz na Kolele Maze kutambuliwa huko.

Umaarufu wa Mapangala ulimwezesha kuteuliwa kuwa Balozi wa Heri Njema wa Kituo cha World Wildlife Fund (WWF) kinachojishughulisha na hifadhi ya mazingira, misitu na wanyama waliomo hasa sokwe mtu.

Tayari ametoa kibao cha Les Gorilles des Montagnes kinachoelezea umuhimu wa kuwalinda sokwe katika misitu ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo na sehemu nyinginezo barani Afrika.

Alikuwa miongoni mwa wasanii waliompigia debe Rais Barack Obama katika kampeni za Marekani za mwaka 2008. Aliimba �Obama Ubarikiwe�. Kibao hicho pia kilipendwa mno hapa nchini.

Mapangala alizaliwa katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo mwaka 1956 na alikulia huko alikoanzia pia shughuli za muziki.
Aliimbia bendi mbalimbali zikiwamo Bariza, Super Tukina, Super Bella Bella na Saka Saka.

Mwaka 1975 alihamia Kampala, Uganda kwa mwaka mmoja kabla ya kuja Nairobi alikoanzisha bendi ya Orchestra Virunga mwaka 1981.
MWISHO.